𝐀𝐉𝐀𝐋𝐈 𝐘𝐀 𝐋𝐎𝐑𝐈,𝐋𝐀𝐔𝐀 𝐖𝐀𝐓𝐔 𝟏𝟏 𝐓𝐀𝐍𝐆𝐀.

Watu 11 wamefariki dunia na wengine 13 kujeruhiwa katika ajali iliyotokea usiku wa kuamkia leo Kijiji cha Chang'ombe Kata ya Segera wilayani Handeni, Mkoa wa Tanga.

Ajali hiyo imetokea baada ya basi aina ya Tata kupinduka na baadaye wananchi kujitokeza kusaidia ndipo lori linalodaiwa kufeli breki likawagonga.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Batilda Burian amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo iliyotokea Januari 13, 2025 na kusema miili imehifadhiwa Hospitali ya Wilaya Korogwe.

Amesema tayari baadhi ya miili imeshatambuliwa na majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu, huku taratibu za kusafirisha miili kwa gharama za Serikali ikiendelea.

Comments

Popular posts from this blog

SAFARI YA KIFAHARI KUTOKA GEITA HADI DAR ES SALAAM NA SHIGAKA LUXURY.

𝐖𝐚𝐬𝐢𝐟𝐮 𝐊𝐚𝐦𝐢𝐥𝐢 𝐰𝐚 𝐁𝐚𝐬𝐢 𝐥𝐚 𝐒𝐜𝐚𝐧𝐢𝐚 𝐌𝐚𝐫𝐜𝐨𝐩𝐨𝐥𝐨 𝐆𝟕 – 𝐊𝐢𝐰𝐚𝐧𝐠𝐨 𝐜𝐡𝐚 𝐊𝐢𝐟𝐚𝐡𝐚𝐫𝐢 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐔𝐬𝐚𝐟𝐢𝐫𝐢 𝐰𝐚 𝐊𝐢𝐬𝐚𝐬𝐚

🚌 Ally’s Star Bus – Dragon Navigator: Mabasi ya Kisasa Yenye Teknolojia ya Ufuatiliaji wa Juu Tanzania